Tuesday, October 9, 2012

VIONGOZI WAIHAMA CHADEMA NA KUJIUNGA NA CCM

Na Steven Augustino, Tunduru
VIONGOZI wa Chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) katika Kata ya Ligunga Wilayani Tundudru Mkoanai Ruvuma umejiengua katika chama hichona kujiunga na Chama cha Mapinduzi CCM.

Pamoja na kukihama chama hicho na kukabidhiwa kadi mpya za chama cha Mapinduzi,Viongozi hao wametamba kukisambaratisha kabisa chama hicho na kuhakikisha kuwa kata hiyo ambayo inaongozwa na Diwani wa Chadema kwa miaka 7 sasa inarejea mikononi mwa chama tawala katika uchaguzi mkuu ujao.

 Tukio lilijitokeza Katika Hafla ya kumakaribisha na kumpongeza Bw. Ajili kalolo  kwa kuwa mshindi wa nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) taifa (NACK) iliyofanyika katika Kijiji cha Jakika Wilayani humo.

Wakitangaza uamzi huo aliyekuwa Mwenyekiti Chadema Kata ya Ligunga Mwenye Akwitanda (Bw.Mohamed Msusa )alisema kuwa yeye pamoja na viongozi wenzake amabo walikihama chama cha Mapinduzi mwaka 2000 kutokana na kero za ubabe na sera kandamizi za viongozi walio ondolewa ndani chama hicho katika uchaguzi uliopita na kwamba kurudi kwao kumetokana na kuamini kuwa hivi sasa chama hicho kupitia mjumbe huyo kitaendesha bila ubaguzi.

Upande wa Bw.Dinani Nambala aliyekuwa na nyadhifa za Mwenyekiti wa Vijana wa Chadema katika kata hiyo na Mjumbe wa mkutano Mkuu Chadema Taifa alisema kuwa kero kubwa ya wanachama hao kuihama CCM mwaka 2000 ilitokana na Uongozi wa Wilaya hiyo kukata Jina la Mgombea ambaye alikuwa ameshinda katika kura za maoni na kuwachaguliz mgombea.

Akifafanua taarifa hiyo Bw. namala alisema kuwa katika uchaguzi huo Bw. Kazembe Said alishinda kwa kupata kura 80 lakini kutokana na ubabe wa uongozi wa CCM wilaya walipandikiza jila la Bw. Omar Kiinge ambaye katika mkutano huo wa uteuzi alipata kura 12 hali ambayo iliwasukuma kuingia msituni na kumsaidia Bw Kazembe ambaye walimshauri ajiunge na Chadema na kuibuka mshindi katika chaguzi za mwaka 2000 na 2010.

Wengine waliojiengua kutoka chadema ni mjumbe wa baraza la wazizi Wilaya Mwenye Akumgambo, pamoja na waliokuwa wapiganaji na wafadhili wakuu wa Chadema Bw. Hasan Ndalanga, Bi. Mwanahawa Msham.

Akiongea katika hafla hiyo pamoja na kuwapongeza viongozi hao kwa kujenga  imani na kurejea katika chama chao mjumbe huyo ambaye pia ni Sultan wa kanda ya Kusini Bw. Ajili Kalolo pamoja na mambo mengine aliomba ushirikiano kwa wanachama na wakereketwa wa chama cha mapinduzi kukisaidia chama hicho ili kuludisha imani kwa wananchi na kukihakikishia ushindi katika chaguzi zijazo.

Aidha Bw. kalolo aliwapongeza wajumbne wa Mkutano Mkuu wa CCM Wilaya kwa kumchagua kuwa mjumbe wa Neck Taifa na kuahidi kuwa yupo tayali kupoteza maisha katika kutetea maslahi ya chama hicho na akatumia nafasio hiyo kuomba ushirikiano kwa viongozi wote pindi akatapo tembea na kuhamasisha chama katika matawi,     mashina,Vijiji,kata na Wilaya zikiwa ni juhudi za kukijenga upya chama hicho.

Awali akitoa taarifa za Ushindi huo mshauri mkuu wa Mneck huyo aliyechaguliwa kwa kupata kura  889, Bw. Sekula Matumla alidai kuwa katika kipindi chote cha uongozi wake atamshari kuondoa makundi ndani ya Chama hicho ili kurejesha imani kwa wananchi na kuwafanya kujiunga na CCM na ikiwezekana doa la upinzani katika Wilaya hiyo liondoke kabisa.

Naye  Katibu wa CCM Wilaya ya Tunduru Bw. ramadhan Amer katika hotuba yake alimweleza Bw. Kalolo kuwa nafasi hiyo ameipata kutokana na kujitoa kwake ndani ya chama na kuongeza kwa kuwahimiza viongozi wote kuwajibika katika nafasi zao ili kujenga chama imara kitakacho pata ushindi katika chaguzi za mwaka 2014 na uc haguzi Mkuu wa Mwaka 2015.

No comments:

Post a Comment