Tuesday, October 9, 2012

MAGHALA YA CHAKULA YATEKETEA KWA MOTO TUNDURU


JUMLA ya Magunia 224 ya mahindi, Mpunga na Maharage mali ya wakulima 10 wa Kijiji cha Mbati mashambani yameteketea kutokana na kuchomwa kwa moto uliozuka katika eneo hilo na kuwasababishia hasara ya kukosa chakula na efdha ya kujikimu.
Sambamba na tukio hilo pia moto huo umeteketeza Nyumba Nane pamoja na mali zlizokuwemo ndani zikiwemo Nyumba tano za famila moja pamoja na majirani waliokuwa wakilima wa kijiji hicho.
Taarifa za tukio hilo zinaeleza kuwa moto huo ulizuka majira ya saa nane mchana ambapo katika tukio hilo wakulima hao walikuwa wameenda kufuata mahitaji Kijijini Mbati na kuacha mali hizo  zikiwa na msimamizi mmoja tu aliyefahamika kwa jina la Bw. Said Nyenje hali ambayo ilimuwia vigumu kuziokoa.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo wakulima walioathiriwa na tukio hilo ni Bw.Rashid Ramadhani aliyeunguliwa na maghala mawili alimo kuwa ametunza magunia 52 ya mahindi ya Chakula na Biashara.
Wengine walio athiriwa na mkasa huo ni Bw.Said Nyenje aliye unguliwa Gunia 32 za Mahindi,Bi. Mwanabibi Hashimu gunia 18, Bw. Amanzi Ngaunje magunia 30 na Bw. said Abdalah gunia 19.
Taarifa hiyo pia imewataja Bw. Bakari Chiganisya magunia 5, Bi. Mwanabibi Chalamanda magunia 8 na Bi. Fatuma Musa aliyeunguliwa na debe 37 za mahindi.
Aidha moto huo pia uliteketeza Debe 70 za Mpunga na maharage zikiwemo Debe 56 za mpunga na Maharage debe 14 mali ya wakulima hao
Miongoni mwa mashuhuda wa tukio hilo Bw. Mohamed Magawa alisema kuwa kutokana na Moto huo kuwa mkubwa na kasi walishindwa kuuthibiti na kuendelea kushuhudia wakati mali zao zikiteketea.
Taarifa iliyotolewa na kuthibitishwa na Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho Bw.Athuman Ntila mbali na kukiri kuwepo kwake walisema kuwa tukio hilo limewaathiri kwa kiasi kikubwa wakulima hao pamoja na mfanya biashara aliyekuwa amefanya nao mkataba wa kuyanunua mahindi hayo baada ya kuyakusanya.
Akiongea kwa uchungu kwa niaba ya wahanga hao Bw.Rashid Ramadhani alieleza kuwa hadi sasa hakuna mtu wanaye muhisi na wala hawatarajii kupeleka kesi hiyo Polisi kwa madai kuwa watachunguza wenyewe na kuchukua hatua hata kwa njia za giza akiashiria kuwa wanampango wa kwenda kuloga kwa wataalamu waliopo Nchi jirani ya msumbiji.
Juhudi za kuwatafuta Mtendaji wa Kijiji hicho Bw. Alli Chandu na Diwani wa kata hiyo Bw. Burhan nakaanje ili kuzungumzia tukio hilo hazikuzaa matunda kutokana na Viongozi hao kudaiwa kuwa wapo katika safari za kikazi.

No comments:

Post a Comment