Tuesday, October 9, 2012

DC< ALALAMIKIA UKUBWA WA BEI ZA BIDHAA TUNDURU

Na Steven Augustino, Tunduru

SERIKALI Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma Imeahidi kuunda Tume itakayo saidia kufuatilia na kudhibiti Bei ya Bidhaa zikiwa ni juhudi za Serikali kuwapunguzia mzigo walaji.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Bw. Chande Nalicho wakati akiongea na Wadau wa Maendeleo katika kikao kilichofanyika katika Viwanja vya Ikulu Ndogo mjini hapa.

Akifafanua taarifa hiyo Bw. Nalicho alisema kuwa maamuzi hayo yamefuatia kuwepo kwa mlipuko mkubwa wa Bei za Bidhaa hali ambayo imekuwa ikiwawia vigumu wananchi kumudu kupata mahitaji yao.

Alisema katika tume hiyo ambayo itawashirikisha Afisa Biashara na Mchumi wa halmashauri hiyo  pamoja na mambo mengine viongozi hao watatakiwa kufanya kazi ngumu ya kuzungumza na Wafanyabiashara wote zikiwa ni juhudi za kumsaidia mlaji na kumwezesha kupata bidhaa hizo kwa bei inayo endana na ubora wa bidhaa husika.

Bw. Nalicho aliendelea kufafanua kuwa endapo hali hiyo haitadhibitiwa ipo hatari ya Wafanyabiashara hao kuendelea kujinufausha kwa kupata faida kubwa huku mlaji akipata bidhaa hiyo kwa bei aghali na kumfanya ashindwe kumudu kufanya shughuli nyingine za maendeleo.

“ hali hii inabidi idhibitiwe kwa taarifa zilizopo zinzonesha kuwa Bidhaa zote zilipanda miaka ya 1994/1995 wakati Wilaya hiyo ilipo kuwa na mlipuko wa upatikanaji wa madini ya Vito” alisema Dc, Nalicho .

Sababu nyingine zilizotajwa kuwa zilikuwa ni kikwazo cha upandaji wa bei za bidhaa hizo katika kipindi hicho kuwa ni ubovu wa barabara kutoka Dar- Es Salaam kupitia Kibiti Lindi hali amabyo ilikuwa ikwafanya kufuata Bidhaa zao kupitia njia ya Songea – Dar Es Salaamu na baadae Songea – Tunduru lakini hivi sasa Bidhaa zao hufika kwa urahisi baada ya barabara ya Kibiti Lindi kufunguka.

Alisema baada ya kufunguka kwa barabara hiyo  yenye umbali wa kilometa 800 kutoka Jijini Dar es salaam kupitia Kibiti Lindi wafanyabiashara wote wamekuwa wakipitisha bidhaa zao huko tofauti na zamani ambapo walikuwa wakipitia Songea ambako kulikuwa na umbali za zaidi ya kilometa 1264 na kwamba hivi sasa wafanyabishara hao wanatakiwa kuwa na roho za kibinadamu na kuondoa kisingizio cha ukubwa wa Ghalama za usafiri kwa lengo la kutaka kujilimbikizia faida.

Alisema kutokana na hali hiyo wananchi hawakuwa na mahali pa kukwepea lakini hivi sasa madini hayo yamekwisha hivyo wafanyabiashara pia wanatakiwa kutambua hali hiyo na kuanza kuuza bidhaa zao kwa bei za kawaida na siyo kujilimbikizia faida maradufu kama wanavyo fanya sasa.

Awali akiwasilisha taarifa ya malalamiko hayo katibu wa Umoja wa makanisa Wilayani Tunduru Padre Dominick Mkapa alitolea mfano Bidhaa za Viwandani yakiwemo mabati, saluji na hata vinywaji ambavyo bei zake zipo juu hali ambayo imekuwa ikwawia vigumu wananchi hata kuanzisha shughuli za ujenzi.

 Kwa mujibu wa taarifa hiyo Mfuko wa saluji umeuzwa kwa Bei ya kati ya Tsh. 24,000 na Tsh. 26,000 , Bati Tshi 22,000 hadi Tsh. 28,000 huku bei ya Soda pia ikiwa ni Tsh. 1,000/= na kilo moja ya Sukali ikiuzwa kwa yati ya  Tsh. 2200 na 2400.

Akizungumzia hali hiyo kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Wilaya hiyo Bw. Rashidi Mandoa mbali na kukiri kuwepo kwa hali hiyo alisema kuwa halmashauri yake ipo tayari kuwatoa wataalamu hao.

Alisema wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo watasaidia kufanya utafiti bei kwa kufanya malinganisho ya Bei za Bidhaa hizo katika Wilaya na miji jirani na baadae kutoa ushauri kwa wafanyaabishara wa Wilaya hiyo

No comments:

Post a Comment