Friday, November 30, 2012

MWENYEKITI WA UMOJA WA VIJANA MKOA WA RUVUMA AHAIDI KUTOA MADAWATI NA KUSAIDIA UPATIKANAJIWA ENEO LA UJENZI WA SHULE

 
  Mwenyekiti wa umoja wa vijana chama cha mapinduzi CCM Khalfan Kigwenembe ametoa ahadi hiyo ya kuchangia madawati baada ya risala ilyosomwa shuleni hapo na Mwalimu mkuu wa shule Bi Otilia Mbano kuonesha shule inakabiliwa na tatizo la ukosefu wa madawati na kusababisha wanafunzi hao kukaa chini wakati wa masomo
Akipokea risala kutoka kwa mwl/mkuu
Aidha aliwataka wazazi wa watoto hao kuhakikisha watoto wao wanajiunga na Darasa la kwanza mapema ifikapo  mwaka 2013 ilikuendeleza masomo yao nakufika mbali kielimu huku akitoa mchango wa madaftari kwa wahitimu wote ili kuwapunguzia wazazi mzigo wa kununua vifaa vya kujifunzia pindi watakapo jiunga na darasa la kwanza,hata hivyo bwn:Kigwenembe amehaidi kuwa tafutia eneo la ujenzi wa shule hiyo kwani kwasasa shule hiyo inatumia majengo ya kupanga. 
 
 Akikabidhi vyeti kwa wahitimu
katika mahafari ya tisa ya shule ya mtakatifu teresia iliyopo bombambili mjini Songea wanafunzi 48 wamehitimu elimu ya awali na kutunukiwa vyeti.
 Nibaadhi ya wazazi wakiangalia kwaya kutoka kwa wahitimu ambao ni watoto wao.

No comments:

Post a Comment