Wednesday, March 6, 2013

WANAWAKE WAHIMIZWA KUACHA UKATILI WA KUUA VICHANGA


 Wakati umoja wa akina mama wa Makanisa ya kikristo Duniani yakikemea ukatili wa Kutupa watoto ambao umekuwa ukifanywa na wanawake Mkazi wa Kijiji cha Mchangani mjini Tunduru Mkoani Ruvuma aliyefahamika  kwa jina la Sikudhani Ajali amefariki dunia wakati akijaribu kutoa mimba.

Akiongea kupita mahubiri katika maadhimisho ya maombi ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika katika Parokia ya kanisa la Mtakatifu  maria imakrata Jimbo la TUNDURU masasi  mhubiri kutoka kanisa la KKKT  Jane Ndonde alioneshwa kukerwa kuwepo kwa taarifa nyingi za matukio hayo zinaelezea ukatili mkubwa ukiwemo wa kuua,kutelekeza ,kutumbukiza watoto vyooni na hata kuwazika watoto wao wakiwa wazima kwea visingizio vyo kutelekezwa na waume zao.

Kuhusu tukio jipya la kujiua kwa marehemu Sikudhani ambaye alidaiwa kujiua kwea sababu ya kutelekezwa na mcumba wake ambaye alikuwa akiishi nae Jijini Dar es salaam muhubiri huyo alidai kuwa Marehemu ambaye amewahi kuwa na watoto zaidi ya 3 kabla ya ujauzito huo alichuku uamuzi huo bila kufikiria na mndiyo maana mungu amemlipa kwa mtindo huo.

Kufuatia hali hiyo Ndonde amabye alinukuu maandiko matakatifu  akatumia nafasi hiyo kuwakumbusha wanawake wa Tanzania na Dunia nzima kutimiza wajibu wao na kukemia vitendo vyote viovu kupitia mwongozo waliopewa kutokaa Umoja wa Makanisa Duniani  kupitia kauli mbiu ya mwaka 2013 inayo sema kuwa   “NILIKUWA MGENI MKANIKARIBISHA” Mathayo sura ya 25.35C. 

Aidha katika hutuba huyi pia Bi. Ndonde aliwaasa wakrsto nchini kutakasa roho zao na kutokubali kuingia katika mkumbo wa mapigano ya kidini yanayo lazimishwa kufanywa na waumini wa dini zingine kufuatia daliliza za mapigano hayo kuanza kutokea katika Mikoa ya Kagera na Ruvuma Wilayani tunduru na Zanziobar.  

Akiongea kwa niaba ya wanafamilia juu ya tukio hilo Diwani wa Kata ya Mchangani Bw.Adam Madina alisema kuwa taarfa zinaonesha kuwa Marehemu alichukua uamuzi huo kufuatia msongo wa mawazo uliosababishwa na tukio la mwanaume huyo kuikataa mimba hiyo
Bw.Madina aliendelea kueleza kuwa mbali na wanafamilia kumsihi asiitoe mimba hiyo kwa siku kadhaa alizoishi Mjini hapa baada ya kukimbia ugomvi huo kwa mchumba wake huyo lakini alionekana kuendelea na msimamo wake wa kuitoa mimba hiyo na kuishia kukubwa na umauti.

 Wakizungumzia tukio hilo miongoni mwa mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa baada yamarehemu kukatazwa kufanya jaribio hilo marehemu aliamua kumeza lundo la vidonge akiwa chooni ambako hata baada ya kuziwa hakuweza kupata msaada wa kuokoa maisha yake kiraahisi na kusababisha kifo chake.

Awali akisoma risala ya maadhimisho hayo Mwenyekiti wa jumuiya inayo inayo waunganisha akina mama wa kikristo Wilayani Tunduru  Rehema Ligombaji alisema kuwa maombi hayo yamefanikishwa na waumini kutopka katika makanisa ya Romani katholiki,Angalikana,Bibilia,Rutherani,Moraviani na Kanisa la Upendo Kriosto masihi.

Mwisho

No comments:

Post a Comment