Friday, October 4, 2013

KATIBU WA UWT TAIFA AMINA MAKILAGI AKAMILISHA ZIARA YA SIKU TATU WILAYANI TUNDURU.



Na shekhan mzaina

Katibu wa UWT Taifa MB.AMINA NASSORO MAKILAGI akiotekasalimiana na wananchi wa kjiji cha mchoteka  kata ya mchoteka.
 
Katibu wa jumuiya ya wanawake wa chama cha mapinduzi CCM na mmbunge wa viti maalum  AMINA NASSORO MAKILAGI amemaliza ziara iliyodumu kwa siku tatu katika wilaya ya Tunduru iliyoanza tarehe 1.10.2013 hadi tarehe 3.10.2013.


Katibu wa UWT Taifa MB.AMINA NASSORO MAKILAGI akihutubia wananchi wa kata ya namihungo wilayani Runduru mkoani Ruvuma.

Pichani wanakijiji cha nakapanya wakisikiliza hotuba ya Katibu wa UWT Taifa na  MB. viti maalum AMINA NASSORO MAKILAGI 

Wakati wa ziara yake wilayani humo yenye malengo mbalimbali ya  chama na serikali  amewataka wananchi hususani akinamama kuwapuuza baadhi ya wanasiasa  wanaochochea vurugu katika nchi yetu ya Tanzania kwani amani iliyopo hapa nchini haikupatikana hivihivi bali lipatikana kwa jasho na wananchi hawanabudi kuilinda amani hiyo,hata hivyo AMINA MAKILAGI amewasihi wanawake wa wilayahiyo kuwa mstari wa mbele kulinda amani nchini kwani wakati wa vurugu akinamama na watoto ndio waathirika wakubwa
.
Akizungumzia tatizo la maji ambalo ni tatizo sugu kwamaeneo mbalimbali hapa nchini ikiwemo  wilaya ya Tunduru  amesema serikali inamikakati kabambe ya kutatua tatizo hilo wilayani humo kwani katika bajeti ya mwaka 2013/2014 serikali imezamilia kupeleka huduma ya maji vijijini kwa kuongeza bajet ya wizara ya maji ili kujiondoa na utegemezi wa wahisani kwa kiasi kikubwa katika utekelezaji wa miradi ya maji  na kata za Nakapanya na Namihungo wilayani tunduru zitanufaika na mpango huo.

Kwa kutambua changamoto zilizopo katika sekta ya afya katibu huyo wa UWT taifa ameahidi kutoa msaada wa vitanda vine vya kujifungulia akinamama vyenye thamani ya shilingi milioni mbili na lakinane  kwa vituo vya afya vya Nakapanya na Mchoteka kwa mgawanyo sawa wa vitanda viwili kwa kila zaanati hizo.
 wanachama wapya wa chama cha mapinduzi CCM wakiapishwa wakati wa mkutano wa Katibu wa UWT Taifa MB.AMINA NASSORO MAKILAGI
Katika ziara yake hiyo wilaya humo UWT imeongeza wanachama wapya 127  katika kata tano za wilaya ya Tunduru huku wanachama sita kutoka chama cha wananchi CUF wamerudisha kadi na kujiunga na chama cha mapinduzi CCM.