Wednesday, May 8, 2013

MAJMBAZI YATEKA GARI NA KUPORA ABIRIA TUNDURU

Na Steven Augustino, Tunduru
WATU wawili waliofahamika kwa majina ya Ester gervas (60) na Gervas
Nipala (65) wamelazwa katika hospitali ya serikali ya Wilaya ya
Tunduru na wengine zaidi ya 30 walitibiwa na kuruhusiwa kuendelea na
safari yao baada ya kunusulika kifo katika tukio la gari waliyokuwa
wakisafilia kutekwa na majambazi.

Tukio lilo linalodaiwa kutekelezwa kundo la genge la majambazi hao
lilitokea katika eneo la Kijiji cha Shamba la Bibi katika tarafa ya
Nandembo Wilayani humo.

Wakiongea kwa nyakati tofauti baadhi ya manusula wa tukio hilo
walisema kuwa mkasa huo uliwapata wakati wakisafiri kupitia basi mali
ya kampuni ya Komba Cochi ambalo hufanya safari zake kutoka Wilayani
Tunduru kwenda makao makuu ya mkoa wa Ruvuma mjini Songea.

Hadija Isaa (30),Ester gervas (60) na Gervas Nipala (65) ambao
walikuwa miongoni mwa manusula hao walisema kuwa katika tukio hilo
maharamia hao walipiga na kuvunja kioo cha mbele cha gari hilo aina ya
Toyota DCM lenye namba za Usajiri T729 BRD na kutoa amri ya akuwataka
watoke nda ya gari na kuala chini huku wakiwa wamefumba macho.

Walisema baada ya abiria hao kutekeleza amri hiyo maharamia hao
waliwavamia na kuanza kuwapiga kwa kutumoa mapanga na magongo huku
wakiwasachi na kufanikiwa kuchukua kila walicho kiona kinafaa ikiwa ni
pamoja na kuwapora simu na fedha.

Akinzungumzia hali za majeruhi hao Mganga mfawidhi wa Hosptalai hiyo
Dkt. Joseph Ng’ombo alisema kuwa majeruhi hao wanaendelea vizuri
baada ya kupatima matibabu hayo na kwamba hata hivyo wabado wanhitaji
kuwa chini ya uangalizi wa maafisa tabibu kwa muda Fulani hadi hali
zao zitakapo imarika zaidi.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Deusidedit Nsimeki amedhibitisha
kuwepo kwa tukio hilo na kueleza kuwa ingawa hadi sasa hakuna mtu
aliyetiwa mbaloni tayali jeshi la polisi kwa kushirikia na wasamaia
wema wamekwisha nasa mtandao wa majambazi hao na wamejipanga kwa ajili
ya kuanza kukabiliana nao kwa kuwakamata.

Alisema hata hivyo majamba hayo yalifanikiwa kupora simu za abilia
wachache na fedha tasilimu tsh.195,0000 na kwamba hali hiyo ilitokana
na majambazi hayo kurupushwa na kukimbizwa na Polisi ambao walikuwa
wakiongozwa na kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Tunduru Bw. Amideus
Tesha ambao walienda kwa haraka baada ya kupatiwa taarifa za tukio
hilo kwa ajili ya kuwaokoa abiria hao.
Mwisho